NAMNA YA KUOMBA HATIMILIKI YA ARDHI YA KIMILA.

1.     HATIMILIKI  YA KIMILA NI IPI.

Hati  ya ardhi  ya kimila ni nyaraka  ya umiliki wa ardhi ambayo  inatoa utambuzi maalum wa umiliki wa ardhi. Hizi ni sawa  na hati miliki zile mnazozijua ambazo hutolewa kwa ardhi za mijini japo ipo tofauti kidogo. Moja ya tofauti  ya hati ya kimila na hatimiliki za mijini ni kuwa hizi husimamia ardhi mijini wakati hizi nyingine husimamia ardhi za vijijini.

2.      HATI YA KIMILA HUTOLEWA NA NANI.

Hati  ya umiliki wa  ardhi ya kimila  hutolewa na baraza la ardhi la kijiji( land village council). Kila kijiji  kinalo baraza hili. Pia baraza hili ndilo linalowajibika kwa masuala ya kila siku ya ardhi ya kijiji. Kwa hiyo maombi  yote ya kuomba ardhi au hati ya kimila yataelekezwa baraza hili.

                    KUSOMA ZAIDI NENDA: sheriayakub.blogspot.com

Visit website

Maoni