Aliyekuwa mlinzi wa mbunge sasa ni mbunge

Nimrod Mbithuka Mbai wakati mmoja aliwahi kuwa mlinzi wa wabunge na maafisa wa serikali , lakini baada ya kupata ushindi wa uchaguzi wa Agosti 8 sasa atahudumu kama mbunge kwa kitui mashariki.
Gazeti la Daily Nation nchini Kenya limesema kuwa afisa huyo wa zamani wa polisi alimshinda mbunge aliyepo madarakani na sasa atajiunga na mbunge aliyekuwa akimlinda bungeni baada ya wote wawili kuchaguliwa katika bunge jipya.

Maoni