BOCCO AREJEA MAZOEZINI SIMBA, NIYONZIMA SASA KUANZA KESHO


Haruna Niyonzima sasa anatakiwa kurejea tena mazoezini kesho.

Awali, Msemaji wa Simba, Haji Manara alisema Niyonzima angeanza mazoezi leo sambamba na John Bocco.

Lakini katika mazoezi ya Simba kwenye Uwanja wa Polisi Kilwa Road jijini Dar es Salaam, ni Bocco pekee aliyeanza mazoezi.

“Niyonzima ataanza mazoezi kesho, leo imeshindikana na daktari ndiye aliyemuongezea siku,” kilieleza chanzo.

Niyonzima aliumia katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara akiichezea Simba. Ilikuwa dhid ya Ruvu Shooting na Simba ilishinda kwa mabao 7-0.

Maoni