Madhara ya kuitumia plastiki kwa kuwekea chakula

Kuna hawa ndg zangu wanachemsha mihogo kisha wanaifunikia nailon ili ilainike vzr. Wengine huhifadhi ugali ktk mifuko ya plastic na kuitumbukiza kwenye maji moto ili ugali usipoe, wengine huchemsha supu ya kichwa cha ng'ombe ule ubongo wanautia ktk mifuko ya plastic na kuuchemsha ktk supu hiyo hiyo hadi unaiva ukiwa ndani ya plastic na plastic ndani ya supu. Je, hizi plastic madhara yake kitaalamu yakoje?
JIBU:
Ustumie kabisa vyombo vya plastik kuchemshia au kuwekea vyakula vya moto kama chai, maziwa, supu, maji, ugali nk.
Ugunduzi mpya ambao umethibitishwa hivi karibuni ni kwamba, plastiki inapopata moto huzalisha kemikali iitwayo BPA (Bisphenol A) ambayo ikiingia mwilini husababisha magonjwa mengi sana kwa binadamu nitayataja machache hapa;
1. Magonjwa ya ini
2. Magonjwa hatari ya moyo
3. Kisukari
4. Magonjwa ya kizazi kwa jinsia zote
5. Kuathiri nguvu za kiume
6. Pumu huongezeka kwa wagonjwa Wa pumu.
7. Huathiri mfumo wa fahamu na kusababisha kupoteza kumbukumbu.
Aisee ni mengi mno wapendwa….
Najua kuna atajayesema ooh siku zote hizo watu wanaishi, sawa ila kumbuka yafuatayo;
Zamani mababu zetu wallikula vitu vya asili na kutumia vitu vya asili na ndomana hawakuwa wanaumwa magonjwa ya ajabuajabu
Mababu Wa zamani waliishi miaka mingi kwani hawakuwa vyakula vya viwandani(manmade chemical foods) vyenye kemikali Kali ya sumu. Sijasema usile, we kula kwasababu hamna namna nyingine sasa. Ila zingatia kunywa maji mengi kama bilauri kumi ivi kwa siku, matunda mengi na mboga za majani. Siku hizi kemikali isipopatikana kwenye chakula hata kwenye vyombo ndo kama hivyo tena.
KAZI YA KUFANYA
A). Hakikisha wewe binafsi unapiga marufuku kuweka vyakula vya moto kwenye vyombo vya plastik hapo kwenye familia yako kwanza. Kwani kuna sababu zipi za kutumia vikombe vya plastik au sahani kwa mfano labda? Ona bei ya vyombo vya udongo ilivyo ya chini
B). Jitahidi uwafikishie taarifa hii mama na baba ntilie hata wawili au zaidi , wasihi kwa hekima mkiwa faragha waambie WAOKOE ROHO ZA WATU zisizo na hatia.
C). Share ujumbe huu kwa makundi ya Whatsapp na sehemu zingine unazoweza kuzitumia . Aisee sambaza ujumbe huu kwa wengi kama umechanganyikiwa. Kufanya hivyo utaokoa wengi sana. Kumbuka wengi hawana elimu hii.
KUMBUKA
Madhara ya plastik huonekana kwa muda mrefu (long term effects) unaweza kutumia na kuendelea zaidi ila baada ya miaka 10 ukapata ugonjwa na ukashindwa kujua chanzo. Wengine watasingizia wachawi kumbe mchawi ni mikono yako!

Maoni