Majibu ya Samatta kuhusu tetesi za kusajiliwa na Fenerbahçe

Ikiwa dirisha la usajili Ulaya linaelekea kufungwa, nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta amezungumzia kuhusu tetesi zilizo mhusisha kuijiunga na klabu ya Fenerbahçe inayoshiriki ligi kuu ya Uturuki.

Fenerbahçe walitajwa kutaka kumsaini Samatta kutokea KRC Genk anayoichezea kwa sasa nchini Ubelgiji ili kuziba nafasi ya mshambuliaji wao Robin van Persie ambaye umri wake umekimbia kwa sasa.

“Sina comment juu ya hilo, siwezi kulizungumzia kwa sababu halijatimia na zilikua rumors mimi sikuzisikia, siwezi kulizungumzia liko nje ya uwezo wangu,” Samatta.


Maoni