ROMA MKATOLIKI,arejea na ngoma mpya ibayo itwa ZIMBAMBWE inayo zingumzia mkasa mzima jinsi alivyotekwa,

Rapa Roma Mkatoliki ametusogezea video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Zimbambwe’ katika wimbo huu Roma Mkatoliki amezungumzia mambo mengi kuhusu sakata la utekaji wake na mambo ambayo amepitia kwa siku tatu ambazo alikuwa ametekwa.
Katika wimbo huu Roma Mkatoliki amegusia juu ya kauli ya Mbunge wa Nkasi (CCM), Ally Kessy ambaye alisema kuwa kitendo alichofanyiwa Roma Mkatoliki ikiwa pamoja na kuteswa na kutekwa ni sawa na kudai kuwa msanii huyo amemtukana Rais Magufuli. Hivyo Roma Mkatoliki amesema hana sababu ya kumtukana Rais na kusema yeye anamshtakia kwa Mungu na kudai atahukumiwa kwa mkono wa Mungu.

Maoni