SABABU KUMI KWANINI UACHE KUNYWA POMBE KWANZIA LEO..

kila mwaka watu watu milioni mbili na laki tano wanauawa na pombe duniani, idadi hii inafanya pombe kua moja ya vyanzo vya vifo ambavyo vinazuilika duniani.. pombe huathiri mifumo mbalimbali ya mwili ikiwemo ubongo, mishipa ya fahamu, moyo, maini na hisia za mtu kiujumla.madhara ya pombe hutegemea sana na kiasi cha pombe mtu anachokunywa..
mambo yanayochangia madhara zaidi ya pombe ni jinsia, umri na historia ya familia husika kwenye unywaji wa pombe..yafuatayo ni madhara ya kutisha yanayosababishwa na unywaji wa pombe..
matatizo ya ubongo; unywaji wa pombe kwa kiasi kidogo tu husababisha mtu kushindwa kuongea, kushindwa kusikia, kushindwa kusoma na kukumbuka, na kushindwa kupata balance wakati wa kutembea.madhara madogo madogo kama haya huweza kuisha mtu akiacha kunywa pombe lakini unywaji wa pombe wa muda mrefu huleta madhara makubwa sana ya ubongo ambayo hayatibiki.
hangover za asubuhi; huu ni mkusanyiko dalili nyingi ambazo mtu huzipata asubuhi baada ya kunywa pome usiku wa jana, dalili hizi ni kama kizunguzungu, kichefuchefu, kutapika, kuchoka sana, kiu, uvivu na kushindwa kufanya lolote siku nzima.
saratani; unywaji wa pombe humuweka mtumiaji katika hatari kubwa ya kupata saratani mbalimbali za mwili kama saratani ya koo ya chakula, maini, kongosho na kadhalika. unywaji wa pombe na uvutaji wa sigara kwa wakati mmoja humuweka mtu kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata kansa hizi.
madhara kwa mtoto aliyeko tumboni ; tafiti zinaonyesha watoto wengi wanaozaliwa na matatizo ya moyo, kuzaliwa kabla ya muda, kuzaliwa na viungo pungufu na kadhalika husababishwa na unywaji wa pombe kipindi cha ujauzito.
kuumia na ajari mbalimbali; mtu akishakunywa pombe basi uwezo wake wa kutafsiri na kuamua mambo unakua mdogo, hali hii humuingiza kwenye ugomvi, kuendesha vyombo vya moto kwa uzembe hata kushiriki ngono zembe na watu mbalimbali.
utegemezi wa pombe; kuna watu wanakunywa pombe kila siku, watu hawa jamii huwashangaa sana na kuwadharau ikidhani wanafanya makusudi lakini watu hawa hawawezi kujizuia kunywa pombe sababu miili yao inataka pombe muda wote na mara nyingi watu wengi wanaoanza pombe kabla ya miaka 21 hupata addiction kubwa ya pombe.
kuongezeka uzito; pombe ina kiasi kikubwa cha nguvu kitaalamu kama calories ambayo kimsingi haina faida yeyote, mtu anayenenepa kwa kula chakula angalau anapata unene pamoja na virutubisho muhimu vya mwili vilivyomo kwenye chakula lakini kwenye pombe ni unene mtupu. ukiwaangalia wahudumu wa bar wengi ambao hunywa pombe hovyo hua ni wanene sana na wenye vitambi.
kuishi maisha mabovu ; unywaji mkubwa wa pombe huweza kuathiri uwezo wako wa kifedha, utaalamu uliosomea au kujifunza, na hisia zako. unywaji wa pombe wa muda mrefu huweza kusababisha magonjwa ya akili kama wasiwasi, mgandamizo wa mawazo na kushindwa kuelewana na watu kitaalamu kama antsocial behaviour.
vifo; unywaji wa pombe husababisha vifo vya muda mrefu kutokana na magonjwa au vifo vya ghafla, hii hutokana na kuongezeka kiasi kikubwa cha pombe kwenye damu ambacho husababisha kuchanganyikiwa, kupoteza fahamu na kufa.historia inaonyesha kwamba mashindano mengi ya kunywa pombe duniani yamesabaisha vifo vya ghafla..nakumbuka mtu mmoja aliwahi kunywa kreti nzima ya bia za guiness na akafa hapohapo.
magonjwa yasiyotibika;uywaji wa pombe unasabaisha magojwa yasiyotibika kama presha ya damu, kuharibika kwa maini na kungosho ambavyo havitibiki.

Maoni