Wafuasi wa upinzani washerehekea Kenya

Wafuasi wa kiongozi wa upinzani nchini Raila Odinga wamejitokea katika barabara nyingi mjini Kisumu na Magharibi mwa Kenya maeneo yanayodaiwa kuwa ngome za upinzani.
Mwandishi wa BBC aliwapiga picha wakisherehekea baada ya kiongozi mmoja wa muungano wa upinzani wa NASA kusema kuwa mgombea wao alikuwa ameshinda uchaguzi wa Jumanne.
Muungano huo unapinga matokeo ya tume ya uchaguzi ya IEBC yanayoonyesha kwamba rais Uhuru Kenyatta anaongoza kwa kura.

Maoni