XAVI AIBUKA NA USHINDI KATIKA BAHATI NASIBU KATIKA BENKI YA DOHA



Kiungo Xavi Hernandez ameshinda bahati nasibu ya benki nchini Qatar.

Kwa sasa, Xavi anakipiga katika timu maarufu nchini Qatar ya Al Saad.

Xavi ambaye ni gwiji la Barcelona anayekipiga nchini humo, alishinda euro 229,000 baada ya kufungua akaunti katika benki ya Doha.

Benki hiyo ilikuwa ikiendesha bahati nasibu kwa wateja wake wote waliofungua akaunti.

Maoni