HUYU NDIYE MCHEZAJI BORA ZAIDI KIHISTORIA KUWAHI KUTOKEA NCHINI UGANDA.

MAJID MUSISI:
NI kweli, Philipo Omondi alikuwa noma enzi zake, lakini unaweza kusema nini kuhusu Majid Musisi Mukiibi?
Mshambuliaji huyo aliyezaliwa Septemba 15, mwaka 1967 kabla ya kufariki dunia Decemba 13, mwaka 2005 vyombo vya habari Uganda vimechekecha vikaamua kuweka bayana, huyo ndiye mchezaji bora zaidi kihistoria kuwahi kutokea nchini humo.

Musisi, ambaye ni mchezaji wa kwanza wa Uganda kucheza soka ya kulipwa Ulaya, alikuwa ana majina mawili maarufu ya utani enzi zake, ambayo ni Tyson na Magic. Tyson kwa sababu alikuwa mkorofi na Magic ni kwamba soka yake iliitwa ya miujiza.

Huyo aliisaidia The Cranes kutwaa Kombe la Challenge katika miaka ya 1989 na 1990. Mfumo wa maisha ya kuendekeza pombe, ulimfanya afananishwe na magwiji wa soka duniani akina George Best, Eric Cantona au Paul Gascoigne ‘Gazza’.

Musisi alikuwa ana utajiri miguuni mwake na mabeki kwa pamoja na makipa walikuwa wanamheshimu sana mtu huyo. Alikuwa hashindwi kufanya jambo anapoamua kufanya kwa juhudi zake zote.

Umaarufu wake uliwavutia vijana wengi kucheza soka Uganda na Afrika Mashariki kwa ujumla. Jamaa alikuwa anaijua soka.

Maoni