IGP SIRRO AZUNGUMZA NA ASKARI WA MKOA WA TANGA


Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro (kulia) akizungumza na kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Jonathan Shana walipokutana katika eneo la Msata Bagamoyo wakati akiwa safarini kuelekea mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Picha na Jeshi la Polisi.

 Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro akipokea salamu ya Kijeshi kutoka kwa Mkaguzi wa Polisi, Ali Masumbuko wakati alipowasili katika Kituo cha Polisi wilaya ya Handeni mkoani Tanga leo, akiwa safarini kuelekea mkoa wa Arusha kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Picha na Jeshi la Polisi.

 Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro (wapili kulia) akizungumza na askari wa wilaya ya Handeni mkoani Tanga wakati alipowasili katika mkoa huo leo akiwa safarini kuelekea mkoa wa Arusha kwa ziara ya kikazi ya siku mbili, IGP Sirro aliwataka askari hao kufanyakazi kwa weledi kwa kuzingatia sheria na taratibu. Picha na Jeshi la Polisi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP),  Simon Sirro akiweka saini kwenye kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika kituo cha Polisi wilaya ya Handeni mkoani Tanga leo, akiwa safarini kuelekea mkoani Arusha. Picha na Jeshi la Polisi.

Maoni