JE WAMJUA PHILIP OMONDI ALIYE ISAIDIA UGANDA KUTWAA MATAJI MWAKA 1973 NA 1977.

PHILIP OMONDI:
UGANDA ndio mabingwa wa kihistoria wa michuano ya Challenge, wakiwa wamebeba Kombe hilo mara 12 (1973, 1976, 1977, 1989, 1990, 1992, 1996, 2000, 2003, 2008, 2009 na 2011).

Wapo wachezaji wawili ambao huwezi kuwatenganisha na mafanikio ya The Cranes katika Challenge. Akina nani hao?
Wote hawa wamekwishatangulia mbale ya haki hivi sasa, Philip Omondi na Majjid Musisi.

Phillip Omondi aliyezaliwa mwaka 1957 na kufariki dunia Aprili 21, mwaka 1999 huyu alikuwa mtu hatari sana enzi zake na waliobahatika kumuona wanaweza kukiri juu ya hilo.

Omondi aliyechezea klabu ya Kampala City Council FC kuanzia mwaka 1973 hadi 1979, alipotimkia Sharjah ya Falme za Kiarabu (UAE) alikuwa shukaa wa Uganda hadi kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika.

Omondi aliichezea The Cranes katika fainali za Afrika miaka ya 1974, 1976 na za 1978, ambazo pamoja na kuifikisha Cranes fainali, pia aliibuka mfungaji bora.

Kwenye Challenge, Omondi aliisaidia mno Uganda kutwaa mataji ya mwaka 1973 na 1977.

Katika fainali za mwaka 1978, mkali wa mabao wa zamani wa Uganda, Phillip Omondi aliungana na Opoku Afriyie na Segun Odegbami katika ufungaji bora, kila mmoja akipachika nyavuni mabao matatu. Leo Omondi hayupo duniani, lakini huwezi kuzungumzia historia ya Challenge bila kumtaja yeye.


Maoni