21/2/2018.
Viongozi wote wa Chadema wa Kata ya Sononi Arusha Mjini, wakiongozwa na Gabriel Simbile ambaye alikua ni Mwenyekiti wa Chadema Kata ya Sononi na Massawe Zabroni Kitomaro aliyekuwa Katibu Mwenezi Chadema katika Kata hiyo wamejivua uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM leo.
Aidha kundi kubwa la wanachama wa Chadema wakiongozwa aliyekuwa Naibu Meya wa Arusha Jiji Bwana Msofe wameachana na
Chama hicho na kujiunga na CCM.
Viongozi na Wanachama hao wamepokelewa na Ndg. Humphrey Polepole akiwa kwenye ziara ya kukagua na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015 - 2020 Wilaya ya Arusha Mjini.
Maoni
Chapisha Maoni