LIQUI MOLY YAJIVUNIA KUWAPATIA WATANZANIA BIDHAA ZENYE UBORA

MKURUGENZI Mkuu wa Kampuni ya Liqui Moil Tanzania, Faraja Mkinga akizungumza Mbele ya Wanahabari kuhusiana na Uzinduzi wa bidhaa zao nchini Tanzania,mapema jana jijini Dar Es Salaam.Mkinga alisema kuwa kampuni yao inajisikia fahari kubwa kuwapatia Watanzania bidhaa zenye ubora wakati Taifa likijipanga kuelekea katika uchumi wa kati.

 ''Tanzania imeingia katika mapinduzi makubwa kwenye sekta ya magari na mitambo kwa kuanza kutumia Oili na vilainishi bora na halisi vya kampuni ya Liqui Moly yenye makao yake makuu nchini Ujerumani'',alisema Mkinga. 

Kuhusu kampuni hiyo, Mkinga amesema ilianzishwa mwaka 1957 nchini Ujerumani na inatengeneza bidhaa zaidi ya 4,000 ambazo zinazosambazwa katika nchi zaidi ya 130 duniani na kwa mara ya kwanza sasa zimeanza kupatikana nchini Tanzania kupitia mawakala wao.Pichani kulia ni Mtaalamu wa Mauzo na Masoko kutoka kampuni ya Liqui Moly Tanzania,Nyanzige Nyabero na kushoto ni Mtaalamu kitengo cha Ufundi Harry Hartkorn.

MKURUGENZI Mkuu wa Kampuni ya Liqui Moil Tanzania, Faraja Mkinga akiwaonesha Waandishi wa habari moja ya bidhaa yao mara baada ya kuzindua bidhaa zao mbalimbali nchini Tanzania,mapema jana jijini Dar Es Salaam.MKinga alisema kuwa “Kuna vilainishi vya magari madogo, magari ya usafirishaaji, meli, majenereta, pikipiki, ndege na mashine mbalimbali za viwandani''. 

Pia tuna mpango wa kuhakikisha tunakuwa na mawakala kwa ajili ya bidhaa zetu maeneo mbalimbali nchini Tanzania,” alisema Mkinga. Amewataja baadhi ya mawakala hao ni Jaffary Car Wash( Mikocheni), Fishcrab Auto Care (Kinondoni) , Top Gear (Kinondoni) , 0-60 (Kinondoni) na TFL Garage (Mikocheni) na wote wapo jijini Dar es Salaam.

Mtaalamu wa Mauzo na Masoko kutoka kampuni ya Liqui Moly Tanzania,Nyanzige Nyabero akizungumza mapema jana mbele ya Wageni waalikwa na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa bidhaa zao za Liqui Moly nchini Tanzania.

Baadhi ya Wageni waalikwa na wadau mbalimbali wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri wakati wa uzinduzi wa bidhaa za kampuni hiyo ya Liqui Moly nchini Tanzania.

Baadhi ya Wageni waalikwa na wadau mbalimbali wakifautilia yaliyokuwa yakijiri wakati wa uzinduzi wa bidhaa za kampuni hiyo ya Liqui Moly nchini Tanzania.

Sehemu ya meza kuu wakifuatilia yaliyokuwa yakijadiliwa ukumbini humo mara baada ya bidhaa za kampuni hiyo kuzinduliwa rasmi nchini Tanzania

Chanzo : Michuzi Blog

Maoni