PWANI YAWATAKA WAFANYABIASHARA , KUSAJILI TIN NUMBER KWA TRA PWANI

SERIKALI mkoani Pwani,imewaasa wafanyabiashara, wawekezaji na wenye viwanda ,kuhakikisha wanasajili namba za utambulisho ya mlipa kodi (TIN no) kwa meneja wa mamlaka ya mapato (TRA) mkoani humo, ifikapo machi 30 mwaka huu.

Hatua hiyo itasaidia mkoa huo kunufaika na wafanyabiashara hao ambao wengi wao kwasasa wanalipa kodi katika maeneo ya mikoa waliojisajili .Mkuu wa mkoa huo,mhandisi Evarist Ndikilo alitoa agizo hilo ,mjini Kibaha wakati wa mkutano wa baraza la biashara la mkoa .

Alisema kutokana na wafanyabiashara wengi mkoani hapo kulipia kodi nje ya Mkoa kunasababisha kudidimiza uchumi wa mkoa."Kila mmoja abebe mzigo wake,mchango wetu kama mkoa hauonekani,na hatunufaiki ,unakuta tuna miviwanda mingi lakini wamekata TIN no.Kinondoni, Ilala ,jijini Dar es salaam ,mapato yake yote yanahesabika huko"

"Kwa mujibu wa takwimu za kitaifa mkoa wa Pwani unachangia asilimia 1.6 ya pato la taifa ambalo liko chini, kumbe wafanyabiashara na makampuni hawatulipi kodi kwenye mkoa jambo ambalo sio sawa," alisema Ndikilo.

 Baadhi ya wajumbe wakifuatilia mkutano wa baraza la biashara la Mkoa  wa Pwani

 Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo amekizungumza wakati wa mkutano wa baraza la biashara la mkoa ,mjini Kibaha. (Picha na Mwamvua Mwinyi)

Mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoani Pwani, Abdallah Ndauka ,akionekana pichani akizungumzia masuala mbalimbali ya kibiashara katika mkutano wa baraza la biashara la Mkoa huo.(picha na Mwamvua Mwinyi)

CHANZO : MICHUZI BLOG

Maoni