WATENDAJI TIMIZENI WAJIBU WENU KUONDOA MIGOGORO - IYOMBE

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe amewaasa watendajii wa mkoa wa Manyara kuchukua hatua stahiki zinazohusu masuala ya watumishi ili kupunguza au kuondoa migogoro mkoani Manyara.

Katibu Mkuu Mhandisi Iyombe ameyasema hayo mjini Babati wakati akiongea na watendaji na watumishi wa Mkoa wa Manyara, Halmashauri ya Mji Babati na Halmashauri ya Wilaya Babati kwamba kiwango kikubwa cha migogoro hasa ya ardhi mkoani humo inatokana na baadhi ya watendaji kutotimiza wajibu wao ipasavyo hali wakizingatia sheria na taratibu za nchi.

“migogoro mingi inaanzia Sight (sehemu wanazotwaa ardhi ili kupima) kwa kuleta taarifa iliyo na mapungufu na pia zingatieni sheria za ardhi, migogoro ipungue kwa kwa kutenda”

Pia Mhandisi Iyombe amesema wapo Watendaji ambao wanashindwa kutumia Mamlaka waliyopewa na kuzuia migogoro ya ardhi ambayo inazuilika lakini pia amehoji mbona mipaka ya mikoa na wilaya ipo wazi na kwanini sehemu nyingine za kiutawala, “msilazimishe migogoro ya ardhi kwani tumewapa mamlaka kwa kufanya Ugatuaji wa madaraka (D by D) hivyo amueni”

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe akiongea na watumishi wa Halmashauri ya Babati na Babati Mji katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya Babati wakati wa ziara yake leo

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe akiongea na watumishi wa Halmashauri ya Babati na Babati Mji katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya Babati wakati wa ziara yake leo

Baadhi ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI) walioshiriki ziara ya Katibu Mkuu OR TAMISEMI Mha. Mussa Iyombe wakiwa katika chumba cha mikutano Babati leo

Katika picha ya pamoja ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara Misaile Mussa wakisikiliza taarifa ya Halmashauri ya Mji Babati

Baadhi ya watumishi wa ofisi ya Mkoa wa Manyara, Babati Mji na Halmashauri ya Wilaya Babati wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe alipokuwa akiongea nao mjini Babati leo

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe alipowasili katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Babati kuongea na watumishi leo.

Maoni