Waziri Mwakyembe Akutana Na Wajumbe Bodi Ya Filamu,atemebela Studio Zinazoandaa Kazi Za Filamu,Muziki


Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Bw. Silvester Sengerema (kulia) moja ya kompyuta mpakato kuashiria makabidhiano ya vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa kwa ajili ya kuimarisha majukumu ya Bodi ya Filamu alipofanya ziara katika ofisi za Bodi na kukutana na wajumbe wa Bodi ya Filamu jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kulia) akimsikiliza Mkurugenzi wa Jasons Televisheni (JTV) Bw. Sanstus Mtsimbe (kulia) alipotembelea studio za televisheni hiyo kuangalia namna kazi za filamu zinavyoandaliwa jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo na wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Bw. Silvester Sengerema

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (waliokaa kulia) akimsikiliza Mkurugenzi wa Studio za Wanene Bw. Darsh Pandit (wapili kushoto) baada ya kuangalia baadhi ya kazi zilizoandaliwa na studio hizo wakati wa ziara yake kutembelea studio mbalimbali zinazojishughulisha na uandaaji wa kazi za filamu na muziki jana Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) kiandika maoni yake katika kitabu cha wageni baada ya kutemblea studio za Wanene zilizopo Mwenge wakati wa ziara yake kutembelea studio mbalimbali zinazojishughulisha na uandaaji wa kazi za filamu na muziki jana Jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo na kushoto ni Mkurugenzi wa Studio za Wanene Bw. Darsh Pandit. 

Maoni