WILAYA YA TUNDURU YAPIGWA JEKI UJENZI WA KITUO CHA AFYA NAKAYAYA MKOANI RUVUMA

 Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Juma Homera kulia, akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 25 kutoka kwa  meneja mawasiliano wa Shirika la maendeleo la Petroli Nchini(TPDC) Marie Msellemu kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Nakayaya wilayani humo.

 Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera katikati na kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya  hiyo Chiza Malando kulia,wakifurahia mfano wa Hundi ya shilingi milioni 25  iliyotolewa na Shirikala maendeleo ya Petroli Nchini(TPDC) kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Nakayaya ambacho kinatajwa mara kitakapokamilika kitasaidia kusogeza huduma za matibabu kwa wakazi wa maeneo yanayozunguka  kituo hicho kushoto ni meneja mawasiliano wa TPDC Marie Msellemu.

 Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Juma Homera,akimtembeza meneja mawasiliano wa Shirika la Petroli Nchini Marie Msellemu maeneo mbalimbali ya ujenzi wa kituo cha Afya cha Nakayaya ambacho ujenzi wake umeibuliwa na kuanzishwa na mkuu huyo wa wilaya kwa kutumia wafadhili mbalimbali.Picha na Muhidin Amri

 Sehemu ya ujenzi wa kituo hichocha Afya Nakayaya kiendelea kengwa,kikiwa chini ya simamizi mkbwa wa DC Homera,kituo hicho kinataraiwa kukamilika Septemba mwaka huu 2018. 

 Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Juma Homera kushoo akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni tano kutoka kwa Vinesh Mathew wa korosho Africa  Ltd kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Nakayaya wilayani humo.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma amepokea hundi ya fedha kutoka shirika la maendeleo ya petrol Tanzania TPDC ambayo ilikabidhiwa na Bi Marie Mselemu Mkurugenzi wa Mawasiliano TPDC .

Bi Marie Mselemu aliongozana na wasaidizi wake akimwakilisha Kaimu Mkurugenzi wa shirika la maendeleo ya petroli Eng Musomba, hata hivyo Bi Marie Mselemu alisema walifikia maamuzi ya kuchangia ujenzi wa kituo hicho cha afya cha Nakayaya ili kuunga mkono jitihada za mkuu wa wilaya ndg Juma Zuberi Homera na pia waliandikiwa barua na  DC Homera ambaye aliibua wazo hili kwa lengo la kukabiliana na msongamano mkubwa wa wagonjwa ulioko hospital ya wilaya Tunduru.

Kwa upande wake DC Homera alilishukuru shirika hilo na kaimu Mkurugenzi huyo kwa moyo wa kizalendo walioonesha kwa wananchi wa Tunduru na pia Homera alisema shirika limeunga mkono jitihada za Mhe Rais Magufuli kwa kutekeleza ilani ya CCM kwa vitendo .

Aidha kwa upande wao kiwanda cha korosho cha Tunduru, Korosho Africa wamechangia fedha za kitanzania million 5 Kati ya million 10 walizoahidi kwa ajili ya kutengeneza madirisha ya chuma ya kituo hicho yani (gril) .kituo hicho mpaka sasa kinaendelea kusimamiwa na Mhe Homera na kinatarajia kukamilika mwezi Septemba mwaka huu 2018.

Maoni