KINARA WA UDHALILISHAJI WANAWAKE MKOANI MOROGORO AKAMATWA.

POLISI mkoani Morogoro imefanikiwa kumnasa mtuhumiwa sugu  ajulikanaye kwa jina la Mabula  Mabula  ( 28), maarufu ‘SIX ‘ mkazi wa Kata ya Mji Mpya , ,Manispaa ya Morogoro , ambaye anajihusisha na matukio ya kubora simu kwa njia ya pikipiki , kubaka wanawake , kuwapora mali zao  kisha kuwabaka na kuwapiga picha za utupu .

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro,  Ulrich Matei alisema hayo  kwa waandishi wa habari kuhusu mkakati wa Jeshi la Polisi mkoani humo kudhibiti matukio ya uharifu na uharifu.

Alisema , kufuatia matukio kadhaa ya ukatili wa aina hiyo yaliyolipotiwa Kituo kikuu cha Polisi ndipo timu ya makachero ikiongozwa na wataalamu wa Cyber – Crime pamoja na kikosi cha kupambana na ujambazi walifuatilia suala hilo kicha kufanikisha ukamataji huo.

“ Matukio matano ya wanawake kufanyiwa vitendo vya ukatili yameripitiwa  kituo kikuu cha Polisi na wahusika wameshindwa kumtambua mihusika  na baada ya kumkamata inaimani watu wanajitokeza “ alisema Matei.

Hata hivyo alisema , baada ya kumhoji mtuhumiwa huyo  alieleza mbinu anazotumia kwamba hijifanya yenye ni akari Polisi ambapo huwakamata wanawake nyakati za usiku na kuwasingizia makosa mbalimbali kasha kuwapeleka mafichoni kwenye kiza kinene maneo ya Tumbaku – Pepsi kuwatishia silaha panga , kupora mali walizonazo na kuwafanyia ukatili wa kuwalawiti na kuwapinga picha za utupu.

 Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei (kulia) akitoa maalezo ya mtuhumiwa sugu   ajulikanaye kwa jina la Mabula  Mabula  ( 28), maarufu ‘SIX ‘ (  wapili kushoto fulana nyeusi ) mkazi wa Kata ya Mji Mpya , Manispaa ya Morogoro , ambaye anajihusisha na matukio ya kubora simu kwa njia ya pikipiki , kubaka wanawake , kuwapora mali zao  kasha kuwabaka na kuwapiga picha za utupu , mwingine na ( kwanza kushoto) ni mtuhumiwa wa ununuzi wa simu za wizi,  Ramadhan Salumu A.K.A Miondoko.

 Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei (kulia) akitoa maalezo ya mtuhumiwa sugu   ajulikanaye kwa jina la Mabula  Mabula  ( 28), maarufu ‘SIX ‘ ( kati kati fulana nyeusi ) mkazi wa Kata ya Mji Mpya , ,Manispaa ya Morogoro , ambaye anajihusisha na matukio ya kubora simu kwa njia ya pikipiki , kubaka wanawake , kuwapora mali zao  kasha kuwabaka na kuwapiga picha za utupu .

 Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei (kulia) akitoa maalezo  kwa waandishi wa habari ( hawapo pichani) juu ya watuhumiwa watatu waliopo kushoto wa wizi wa mitandao  waliokamatwa na  simu tisa aina mbalimbali pamoja na laini 57 za mitandano mbalimbali ikiwa na  kurasa sita za kitabu cha kumbukumbu kwa wakala (Log Book ) za mtandao wa Vodacom ambazo zina namba za siku za wateja. ( Picha zote na John Nditi).

Maoni