MBARAZA UVCCM DSM AZINDUA MFUMO WA KIELECTRONIKI KWA SHUGHULI ZA UVCCM MKOA DSM

Mjumbe Baraza kuu UVCCM Taifa Mkoa Dar es Salaam Ndugu Gwantwa Alex mwakijungu Leo jumapili Tarehe 10 March 2018 amezindua Mfumo wa Kanzi Data (Data Base) kwa shughuli za jumuiya ya vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam. 

Kazi kubwa ya mfumo huu itakuwa ni upatikanaji wa taarifa muhimu, usajili wa wanachama wapya, Mfumo wa Malipo ya wanachama na Shughuli nyingine mbali mbali. 


Katika uzinduzi huo pia Ndg. Mwakijungu amekabidhi Laptop 20 zenye thamani ya Tshs 36 Milioni kwa ajili ya kusimamia na kusaidia kikosi kazi cha ukusanyaji Taarifa ya wanajumuiya Mkoa wa Dar es Salaam kwa Katibu wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam ndugu Said Yassin.

Hafla hii imefanyika Ofisi za Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Wajumbe wa Kamati Tekelezaji UVCCM Mkoa wa Dar es salaam chini ya Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa DSM Musa Kilakala, Katibu hamasa Mkoa Saady Khimji, na wenyeviti wa UVCCM wilaya ya Ilala na kigamboni.

Maoni