MKURUGENZI wa Halmashauri wa Temeke jijini Dar es Salaam, Nassib Mmbagga ametoa pole kwa wafanyabiashara wa soko la Mbagala Rangi tatu ambao wamepoteza mali zao baada ya kuungua kwa soko hilo.
Soko hilo ambalo lilikuwa na wafanya biashara zaidi ya 500 lilianza kuteketea usiku wa kumkia leo.
Akizungumza leo,Mkurugenzi amesema Halmashauri imepanga kukutana na wafanyabiashara waliokuwa wakifanya biashara katika soko hilo.
Amesema lengo ni kuangalia ni jinsi gani halmashauri itawasaidia
Vibanda vilivyokuwa vinamilikiwa na wafanyabiasharawa Soko la Mbagala Rangi Tatuvikiwa vimeteketea kwa moto.
Baadhi ya wananchi wakiwa eneo la Tukio.
Maoni
Chapisha Maoni