SERIKALI KUTOA KIBANO KWA WATENDAJI WANAOHUJUMU FEDHA ZA SERIKALI.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amefunga kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara ambapo amewaasa washiriki hao kutumia fedha za Serikali kwa kufuata sheria.

Mheshimiwa Ndalichako alisema Wizara ya Elimu itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Rais,TAMISEMI kwa kuwaadhibu wale wote wanaoenda kinyume na matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Elimu bila ya kuzingatia sheriaa na miongozo ya utekelezaji wake.

“Wizara ya Elimu pamoja na Ofisi ya RAis TAMISEMI itawachukulia hatua Wale wote wataokula fedha za miradi na hawatopelekewa pesa za miradi mingine hadi wakamilishe miradi ambayo haijakamilika na kutoa mchanganua wa matumizi yake,”Amesema

Ndalichako alihamasisha uzingatiaji wa taratibu za fedha kwani Viongozi wa ngazi ya juu hususani Mawaziri wamekua wakijibu tuhuma za ubadhilifu wa fedha kwa wakaguzi wakati hawakuchukua fedha hizo.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akitoa hotuba ya kufunga kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akitoa hotuba ya kufunga kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akijadiliana jambo na Naibu Katibu Mkuu (ELIMU) Ofisi ya Rais TAMISEMI, Tixon Nzunda wakati wa kikao kazi cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu (ELIMU) Ofisi ya Rais TAMISEMI, Tixon Nzunda akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi wakati wa kikai kazi kilichofungwa jana cha Makatibu Tawala Wasaidizi wa Elimu na Mipango ngazi ya Mikoa, Wakaguzi wa ndani wa Hesabu, na Maafisa Elimu Wilaya kutoka Halmashauri zote 186 Tanzania Bara mjini Dodoma.

Maoni