SIKU YA WANAWAKE DUNIANI ILIVYOADHIMISHWA MKOANI TABORA


Mke wa Rais Mstaafu Mama Salma Kikwete akimpongeza Mbunge wa Vitimaalum mkoa wa Tabora Munde Tambwe baada ya kupokea kiasi cha shilingi milioni moja kwaajili ya TIKA huku Mbunge huyo Munde Tambwe akiahidi mbele Mama Salma Kikwete kuchangia jumla ya mifuko Miambili ya Saruji kwa ajili ya Ujenzi wa Mabweni katika Shule za Sekondari za kata manispaa ya Tabora na ujenzi wa uzio Kliniki ya Tabora mjini maarufu Town Clinic. 

Mke wa Rais mstaafu wa awamu ya nne Mama Salma Kikwete akizungumza katika maadhimisho hayo ambapo alisema kuna haja ya kuleta mabadiliko ya kisekta yatakayoharakisha maendeleo kwa Wanawake kupitia kujenga misingi imara ya kupata elimu bora itakayotoa fursa kwa Wanawake kuajiriwa na hata kujiajiri wenyewe. 

Mbunge wa Vitimaalum mkoa wa Tabora Munde Tambwe akizungumza katika Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wanawake zilizofanyika kimkoa mkoani Tabora,katika maadhimisho hayo Munde aliwalipia Kadi za matibabu maarufu TIKA Wanawake wasio na uwezo Miamoja wanaoishi manispaa ya Tabora akiwa anakamilisha idadi kama hiyo kwa Wanawake wengine mia moja kwa kila Wilaya za mkoa wa Tabora ambazo ni wilaya saba. 

Maadhimisho ya Siku ya wanawake duniani mkoani Tabora ambapo Mama Salma Kikwete alikuwa mgeni rasmi iliyofanyika viwanja vya Chipukizi mjini Tabora. 

Gwiji na Msanii mkongwe wa muziki wa Taarabu nchini Malkia Khadija Kopa akitumbuiza katika maadhimisho hayo mjini Tabora katika viwanja vya Chipukizi. 

Maoni