WAZIRI UMMY AENDELEA NA ZIARA YAKE WILAYANI ILEJE AFUNGUA KITUO CHA AFYA NA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI


 Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  akitoa udongo wakati wa  uchimbaji wa msingi katika ziara yake ya ufunguzi wa kituo cha Afya cha Mtura kata ya Lubanda wilaya ya Ileje.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  akiendelea na ukaguzi wa ujenzi wa kituo cha Afya Mtura kilicho katika kata ya Lubanda Wilaya ya Ileje mkoa wa Songwe

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  akielekea eneo la gari lililokwama kutokana na changamoto ya Barabara, wakati akiwa katika ziara yake ya ufunguzi wa kituo cha Afya cha Mtura kata ya Lubanda wilaya ya Ileje. Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ileje Haji Mnasi.Kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Kheri Kagya

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Ileje na watumishi wa Serikali (hawapo kwenye picha) wakati akiwa katika ziara yake ya ufunguzi wa kituo cha Afya cha Mtura kata ya Lubanda wilaya ya Ileje.

 Wananchi wa kata ya Lubanda katika kijiji cha Mtura wilaya ya Ileje wakimsalimia Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu.

Maoni