Al Shabaab Waua Wanajeshi Wanne Kutoka Uganda


Wanajeshi wanne wa jeshi la Uganda katika kikosi cha kulinda amani  nchini Somalia AMISOM wameauwa katika shambulizi lililotkelezwa na wanmagambo wa kundi la kigaidi la al shabaab. Shambulizi hilo limetekelezwa Jumapili.

Msemaji wa jeshi la Uganda  Richard Karemire  aliambia shirika la habari la Anadolu kuwa  wanajeshi wanne wa Uganda katika kikosi hicho cha kulinda amani Somalia wameuawa na wengine 6 wamaejeruhiwa.

Shambulizi hilo limetekelezwa katika kambi inayopatikana Bula Marer.

Kwa mujibu wa msemaji huyo , wanagambo wa kundi la al shabaab  wapatao 30  waliuawa katika operesheni walipokuwa wakijaribu  kushambulia kambi tofauti za jeshi la ushirika la kulinda mani nchini Somalia AMISOM.

Kambi zilizokuwa zikilengwa na magaidi hao ni kambi ya Qoryoley, Buulo Marer na Golwen.

Maoni