BARCELONA WANG'OLEWA LIGI YA MABINGWA, MESSI ATIA HURUMA ROMA

Lionel Messi akitembea kinyonge baada ya Barcelona kufungwa 3-0 na wenyeji, Roma katika mchezo wa marudiano wa Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa Jumanne na kutolewa kwa mabao ya ugenini baada ya sare ya jumla ya 4-4 kufuatia awali kushinda 4-1 kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Olimpico mjini Roma. Mabao ya Roma leo yamefungwa na Edin Dzeko dakika ya sita, Daniele De Rossi dakika ya 58 na Konstantinos Manolas dakika ya 82.

Maoni