Eneo la mto Koga Lilivyo kufuatia mvua za masika zinazoendela kunyesha hali iliyosababisha bara bara ya Tabora Katavi kufungwa
Mkuu wa Mkoa wa KataviMeja Jeneral Mstaafu Raphael Muhuga amesema barabara ya Mpanda–Tabora imefungwa kwa muda usiojulikana kuanzia Aprili 14,2018.
Muhuga ametoa kauli hiyo katika mkutano wa hadhara unaofanyika katika uwanja wa Azimio mjini Mpanda kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi ambapo hata hivyo mkutano huo umeahirishwa baada ya mvua kunyesha na kupangwa kuitishwa baadaye ili kujibu malalamiko ya wananchi.
Muhuga amesema barabara hiyo imefungwa baada ya maji kujaa barabarani kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha na hivyo kuhatarisha maisha ya wasafiri.
Kwa upande wake mkuu wa mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa majini na nchi kavu Sumatra Mkoani Katavi Amani Mwakalebela amesem kutokana na barabara kuharibika kwa kiasi kikubwa,wenye mabasi watalazimika kusafirisha abiria kupitia mkoani Kigoma au Mbeya.
Mwaka 2016 barabara ya Mpanda – Tabora ilifungwa baada ya kukatika kwa daraja la mto Koga ambapo karibu watu kumi walipoteza maisha baada ya gari kusombwa na maji.
Chanzo:Issack Gerald
Maoni
Chapisha Maoni