Wakazi na wakulima wa eneo la Mpanda Hoteli Kata ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wameiomba mamalaka ya maliasili kuondoa viboko walio jirani na makaz yao kutokana na kutishia maisha
Wakizungumza na Mpanda radio wananchi hao wamesema kuwa wanahofia zaidi maisha yao baada ya viboko hao kuvamia eneo la mto Mpanda
Kwa upande wake Mkurugenzi wa manispaa ya Mpanda maiko znyungu ameahidi kulishulikia suala hilo kwa kuwasiliana na mamalaka ya maliasili
Kuzagaa kwa wanyama hao hali imetajwa kuwa ni kuendelea kunyesha kwa mvua za masika huku wanyama hao wengine wakitajwa kusombwa na maji.
CHANZO:Ezelina Yuda
Maoni
Chapisha Maoni