Katibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahman Kinana leo ameongoza ujumbe wa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya zake, kuzuru ubalozi wa Afrika ya kusini nchini Tanzania kusaini na kutoa pole kufuatia kifo cha Mke wa Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini na mwanaharakati Mama Winnie Mandela aliyefariki 2/04/2018 Johanasburg nchini Africa ya Kusini.
Katibu Mkuu amefuatana na Mwenyekiti wa UWT Mama Caudensia Kabaka, Katibu Mkuu wa jumuiya ya Wazazi Maalim Seif Shaaba, Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka, Katibu wa NEC Siasa na uhusiano wa Kimataifa Kanal mstaafu Ngemela Lubinga, Naibu Katibu Mkuu wa UWT na Naibu Katibu Mkuu wa jumuiya ya Wazazi.
Maoni
Chapisha Maoni