Miaka 9,jela kwa tuhuma za kuwauawa wanaye wawili.

Mahakama nchini Ujerumani katika mji wa Halle leo April 5, 2018 imemhukumu mwanamke wa miaka 46 kwa makosa ya kuua watoto wake wawili.

Mahakama imemhukumu kifungo cha miaka tisa na nusu jela kwa kosa hilo. Inaripotiwa kuwa mwaka 2004 mwanamke huyo alijifungua mtoto wake wa kwanza lakini baadaye alimuua na kuweka mwili wake kwenye jokofu (freezer).

Mwaka 2008 pia mama huyu alijifungua mtoto wa kike lakini kwa mara nyingine tena alimuua na kuweka mwili wa mtoto huyo kwenye freezer kama ilivyokuwa kwa mtoto wa kwanza.

Maoni