Wananchi wa mtaa wa Airtel katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wameiomba Serikali kuwasaidia kuboresha daraja ambalo limekuwa likijaa maji katika kipindi cha mvua
Wameyasema hayo wakati wakizungumza na Mpanda Radio na kusema kuwa daraja hilo limesombwa na kujaa maji na kusababisha wananchi kushindwa kuvuka na wengine kusombwa na maji hayo.
Hivi karibuni wakala wa barabara za mjini na vijijini TARURA mkoani Katavi imesema kuwa upo mpango wa kukarabati barabara na madaraja yote ya mijini na vijijini ili kupunguza ubovu wa miundombinu.
Tatizo la miundombinu maeneo mengi mkoani Katavi kipindi cha masika limekuwa kikwazo kwa wananchi kushindwa kufanya shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
Maoni
Chapisha Maoni