MVUA ZAKWAMISHA WASAFIRI.


Baadhi ya wafanyabiashara wa usafirishaji abiria mjini Mpanda wamelazimika kusitisha huduma kutokana na ubovu wa miundombinu.

Mpanda Radio imefika katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani mjini Mpanda na kuzungumza na baadhi ya wahudumu wa kampuni za usafirishaji ambazo zinatumia barabara ya mpanda-tabora.

Kwa sasa magari yaliyokuwa yakitumia barabara hiyo yameamriwa kutumia barabara ya Mpanda-Kigoma ambapo wafanyabiashara hao wamesema kuwa wanalazimika kuongeza nauli kwa shilingi elfu kumi hadi elfu kumi na tano kwa kila safari kwa kuwa umbali wa safari umeongezeka

Hata hivyo wamesema kuwa barabara mbadala ya kupitia uvinza nayo haipo kwenye hali nzuri kitendo kinachosababisha ugumu wa safari.

Mwishoni mwa wiki iliyopita mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Rafael Muhuga alitangaza kufungwa kwa barabara ya Mpanda-Tabora baada ya barabara hiyo kujaa maji.

Maoni