Watu 18 wameuawa na wengine 84 wamejeruhiwa.


Takriban watu 18 wameuawa na wengine 84 wamejeruhiwa katika shambulizi lililofanywa na waasi wa Boko Haram waliokuwa wakipambana dhidi ya wanajeshi wa serikali karibu na mji wa kaskazini mashariki wa Maiduguri usiku wa kuamkia leo.

Shirika la kitaifa la kushughulikia maafa na matukio ya dharura nchini Nigeria limesema kufikia sasa wamepata miili 18 kutoka vijiji viwili vya Bale Shuwa na Bale Kura vilivyoko mkoa wa Maiduguri na kuongeza wahanga hao waliuawa walipokuwa wakijaribu kukimbia mapigano yanayojiri kati ya waasi na wanajeshi.

Maiduguri ambao ni mji mkuu wa jimbo la Borno ndiyo chimbuko la kundi hilo la waasi la Boko Haram ambalo lilianza uasi miaka tisa iliyopita kaskazini mashariki mwa Nigeria.Kiasi ya watu 20,000 wameuawa tangu wakati huo na karibu milioni mbili kuachwa bila ya makazi.

Maoni